NEW UPDATES

Christiano Ronaldo akabidhi T-shirt ya kutimiza magoli 100 ulaya

Cristiano Ronaldo amekiri kuwa hakuwahi kufikiria atakuwa mchezaji wa kwanza kufunga magoli 100 katika michuano ya Ulaya, wakati alipoanza soka lakini amesema amefurahishwa mno na mafanikio ya hayo.

Ronaldo alifikisha magoli hayo baada ya kuifungia Real Madrid magoli mawili Alhamis katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ulioishia kwa ushindi wa magoli 2-1.

Mshambuliaji huyo Mreno alikabidhiwa fulana ya kumbukumbu ya kufikisha idadi hiyo ya magoli na rais wa Real Florentino Perez hapo jana kwa kufanikiwa kufikia idadi hiyo ya magoli na yeye kusema amefarijika mno.

No comments

https://instagram.com/bakihotnews?utm_medium=copy_link