NEW UPDATES

MTOTO ALIYEPATA DEGREE AKIWQ NA UMRI MDOGO DUNIANI.

MFAHAMU MTOTO ALIYEPATA ‘DEGREE’ AKIWA NA UMRI MDOGO DUNIANI

Michael Kearney ambaye ndiye mtoto wa kwanza duniani kuongea akiwa na umri mdogo  alipokea shahada yake ya kwanza akiwa na umri wa miaka 10 tu.

Kernry ambaye alianza kuongea akiwa na umri wa miezi minne aliwashangaza watu kwa maendeleo yake makubwa aliyoyaonesha akiwa na umri mdogo kabisa.

Akiwa na umri wa miezi 10 alikuwa tayari anajua kusoma na alipofikisha miaka minne alifanya vizuri kwenye mitihani ya majaribio ya hisabati aliyopewa.

Kwa mujibu wa wanasaikolojia, watoto wa aina yake hutokea mara chache na kuna baadhi ya nchi au sehemu hawajawahi kutokea kabisa.

Michael Kearney alizaliwa mwaka 1984 huko Hawaii Marekani na ni mmoja wa watoto waliovunja rekodi ya dunia kwa kuwa na akili nyingi akifanikiwa kumaliza chuo kikuu katika umri mdogo pamoja na kufundisha chuo kikuu akiwa na umri mdogo kabisa.

Siku za mwanzo za maisha yake mtoto huyo alikuwa akijifunzia nyumbani huku akipata msaada kutoka kwa wazazi wake ambao walikuwa ni wamarekani wenye asili ya Japan.

Dada yake aliyeitwa Meghan naye aliweza kumaliza chuo kikuu akiwa na umri wa miaka 16 tu.

Kwa mujibu wa profesa wa saikolojia Martha J Morelock, Kearney alisaidiwa na wazazi wake kufahamu mambo mengi na alikuwa na uwezo wa pekee wa kuelewa.

Mtoto huyo alizungumza neno lake la kwanza akiwa na umri wa miezi minne. Akiwa na umri wa miezi sita aliweza kumwambia daktari wao “nina maumivu kwenye sikio langu la kushoto”

Akiwa na umri wa miaka minne, alipewa jaribio la Hisabati na shule ya Hisabati ya Johns Hopkins bila kuwa amesoma kwa ajili ya mtihani na alifaulu kwa kiwango cha juu.

Alisoma katika shule ya San Marin High School iliyopo Novato huko California kwa mwaka mmoja na alimaliza akiwa na umri wa miaka sita mwaka 1990. Mwaka 1994 walikuwa wakishiriki kwenye kipindi maarufu cha televisheni kilichoitwa ‘Tonight show’

Alijiunga na shule ya Santa Rosa Junior college iliyopo Sonoma California na alimaliza akiwa na umri wa miaka minane, akichukua masomo ya Sayansi ya madini. Mwaka 1993 familia yake ilihamia Alabama na alifanikiwa kuingia kwenye rekodi ya kitabu cha ‘Guiness book of world  records’ kuwa mtu mwenye umri mdogo zaidi duniani kumaliza chuo kikuu na akiwa na miaka 10, akichukua Shahada ya masuala ya kale.

Alimaliza Shahada yake ya pili (masters) ya Kemia kutoka chuo kikuu cha umma cha Tennessee huko Marekani akiwa na miaka 14.

Utafiti wake aliofanya ili aweze kupata shahada hiyo ya pili ulikuwa na kurasa 118 uliwashangaza wengi na alivunja rekodi ya dunia kwa kuwa mtu wa kwanza mwenye umri mdogo kuweza kupata Shahada ya pili duniani.

No comments

https://instagram.com/bakihotnews?utm_medium=copy_link